Sunday, March 2, 2014

Afya ya Akili ni nini?





Tafsiri ya dhana ya afya ya akili

1.    Ni hali chanya kihisia na kisaikolojia inayomwezesha mtu kutumia uwezo wake wa kufikiri na kutawala hisia zake, katika kukabiliana na masuala mbalimbali ya kijamii, pia kuhimili changamoto mbalimbali za maisha ya kila siku.

2.    Uwezo wa kufurahia maisha, kujiamini, na kujikubali,  kuwakubali watu wengine, kujithamini na kuwathamini wengine, kuonyesha upendo na kuweza kupokea upendo kutoka kwa wengine, mawasiliano na ushirikiano mzuri kijamii, kuwajibika na kutekeleza majuku vizuri; ni mambo yanayoashiria kuwepo kwa afya bora ya akili.

Fikra, hisia na matendo ya mtu vinaashiria hali ya afya yake ya akili.
(Kwa mfano: Wewe unakabiliana vipi na msongo wa maisha?)
Mtizamo wako juu ya ubinafsi wako, mtizamo wako juu ya maisha unayoishi na unavyohusiana na wale uanoshirikiana nao katika maisha yako.
 Mfano: Je! Wewe unahusiana vipi na watu wengine?
Namna unavyopima njia kadhaa za kupata ufumbuzi wa suala lililo mbele yako.
 (Mfano: namna unavyofanya maamuzi katika maisha yako).

Nguzo muhimu kuhusu afya ya akili

  1. Fikra zako
  2. Hisia zako
  3. Matendo yako

Fikra zinazotawala mawazo yako


1. Mfumo wa kufikiri ni sehemu muhimu ya afya yako ya akili. Ni vizuri ukajitambua namna     fikra zako zinavyotafsiri masuala mbalimbali katika mazingira yako. (Kwa mfano: umekutana na rafiki yako akiwa na rafiki mwingine na inaelekea wanafurahiana na kucheka  pamoja)
2. Ni vizuri kujichunga aina ya mawazo yanayotawala fikra zako. Je! Unaruhusua fikra hasi    zitawale mawazo yako?
3. Fikra zinazotawala mawazo au ufahamu wako ni hutatawala mweleko wa hisia zako

          Hisia au namna Unavyojisikia

1.    Mzuka,   Furaha, Upendo, Utulivu, Amani
2.    Chuki, Wivu, Hasira, Wasiwasi, Woga, Huzuni

Wivu
Huzuni

Wivu




Huzuni



Mzuka






Hasira

Je! Unajisikia vipi? Tambua hisia zako

1.    Hisia ni sehemu muhimu ya ufahamu wa mtu kisaikologia. Fikra zako zinasababisha namna unavyojisikia. (Kwa mfano; ukigundua jengo hili linawaka moto …….)
2.    Iwapo Mawazo yahayotawa ufahamu wako ni hasi, utakuwa na hisia za wasiwasi, woga, pengine chuki and wivu.
3.    Ni muhimu kujitambua hisia zako. Mfano; Ninajisikia mwenye hasira, sina raha. Ni vizuri kujiuliza hii hasira inatoka wapi au inatokana na nini. Unafikiria nini kuhusu tukio fulani? Tukio la kawaida kwa watu wengine kwako linaweza kuwa na maana mbaya au hasi.
4.    Jiulize kama tukio husika linahalalisha wewe uwe na hasira au chuki.

Vitendo hutokana na mawazo na hisia zako.

Fikra zako zinaleta mabadiliko katika hisia zako, na hii inakuwa chimbuko la yale utakayotenda. Mifano; ………..

KUJIFUNZA KUTOKA MAISHA YA UTOTO

  1. Tangu utotoni tunajifunza kwamba matendo Fulani yana matokeo mabaya kwetu. Kwa mfano; Ukigusa kitu cha moto unaungua na kupata maumivu, au ukifanya kosa unaweza kuadhibiwa.
  2. Kwa mfano huo, ni vizuri pia tukajua kwamba fikra na hisia mbaya lazima zitakuwa na matokeo katika maisha yetu. Kama ni fikra mbaya zinazoambatana na hisia mbaya, matokeo yake nayo yatakuwa mabaya.
TAZAMA MIFANO MICHACHE

Hali ya afya ya akili huleta mabadiliko katika uhusiano na watu wengine
      Matatizo ya afya ya akili yanaathinri uhusiano na familia, ndugu, wapenzi, majirani, mwajiri, …….


Matatizo ya afya ya akili yanaweza kuathiri uwezo wako wa kukabiliana na masomo

  1. Inaathiri uwezo wa kufuatilia masomo kwa makini
  2. Inaathiri uwezo wa kutoa kipaumbele kwa masuala muhimu
  3. Inaweza kuathiri tabia na mwonekano wako darasani
  4. Uwezo wa kuweka mambo kwa mpangilio mzuri kubadilika
  5. Pia uwezo wa kujenga hoja na kuiwasilisha kwa ufasaha inaweza kuathirika.

Afya mbaya ya akili kama chanzo cha matatizo mengine:

  1. Kujaribisha dawa za kulevya
  2. Ngono  na wapenzi wengi kama namna ya kujiliwaza
  3. Kuwa mkorofi na mgonvi
  4. Kujiingiza katika tabia hatarishi

Namna ya kuimarisha afya ya akili

  1. Kula na kunywa maji ya kutosha
  2. Fanya mazoezi ya viungo angalau mara tatu kwa wiki
  3. Jali afya yako kila siku (jitambue na epuka vishawishi vya kula au kunywa vitu vinavyoathiri afya yako)
  4. Jipe muda wa kutafakari maisha yako mara kwa mara
  5. Muda wa kulala uwe wa kutosha – wastani wa saa 7 kwa siku
  6.  Chukua hatua madhubuti kukabiliana na dalili za msongo
  1. Kucheza au kushiriki matendo ya kujifurahisha – tafuta fursa za kujifurahisha kwa namna ambayo inajenga afya yako na kupunguza msongo.
  2. JITAMBUA – Fahamu na tawala fikra na hisia zako
      Unaweza kuanzisha daftari la kuweka kumbukumbu za fikra na hisia mbalimbali ambazo unaona ni muhimu katika maisha yako.
      Jitambue unapokuwa na fikra au hisia ambazo ni tofauti na kawaida yako
      Wakati mwingine unatakiwa kusema hapana kwa baadhi ya majukumu hasa pale yanapokuwa mengi mno kulingana na muda ulio nao.
      Tenga muda wa kutuliza akili yako, hakuna redio, TV na simu unaizima kukupa muda wa utulivu katika nafsi yako.


Nifanyeje kulinda afya yangu ya akili?

1.    Tambua dalili za mabadiliko:
      Namna unavyofikiri (aina ya mawazo yanayotawala akili yako)
      Katika hisia zako (unajisikia tofauti na kawaida yako – labda una wasiwasi, huzuni, au unapatwa hasira bila sababu kubwa)
      Unaonyesha matendo ambayo ni tofauti na kawaida yako
      Jifunze mbinu za kupunguza msongo wa mawazo na kuepuka tabia ambazo ni hatarishi kuleta msongo siku zote za maisha yako.
2.    Ni muhimu kujua ni lini na wapi unaweza kupata msaada iwapo utakuwa na msongo.
      Pata huduma mapema iwezekanavyo
3.    Pata huduma kutoka kwa mtaalam na pengine upate rufaa



ASANTENI KWA KUJIFUNZA

Friday, February 28, 2014

Afya ya Akili Yako


“Burnout”
Kujisikia dhaifu / mchovu sana
kimwili na kiakili.

Mwili na akili kuishiwa nguvu ina maana gani?
(“burnout” ina maana gani?)
Hali ya kuishiwa nguvu mwilini, fikra na hisia kuwa za unyonge kutokana na kujituma mno kuliko uwezo  alio nao mtu. Mtu anajitoa sana kuwajibika au kuhudumia bila kujipa nafasi ya kupumzika.

Msongo unapozidi uwezo wako
1.     “Burnout” ni sehmu ya kukabiliana na hali ya msongo. Inatokea iwapo hali ya msongo inakuwa kubwa mno na kwa muda mrefu.
2.     “Burnout” ni hali ambayo inaathiri ufanisi wa mwili na akili.
3.     Mambo yanapokuwa magumu, mara nyingi tunasahau kujali na kulinda afya zetu. Tunaposahau kulinda afya zetu na kuruhusu hali ya msongo kutawala maisha yetu kwa muda mrefu, tunajiweka katika hatari ya kupata BURNOUT.

DALILI ZA “BURNOUT”
1.     Kimwili
2.     Akili /Hisia
3.     Mwenendo /matendo/


Mabadiliko mwilini
1.     Uchovu /kuishiwa nguvu
2.     Kukosa unsingizi au kulala sana
3.     Misuli ya mwili kukaza na kuuma
4.     Hamu ya kula kupungua au kuongezeka
5.     Maumivu ya kichwa
6.     Kupungukiwa tamaa ya kujamiana
7.     Kujisikia mgonjwa mwili mzima
8.     Mapigo ya moyo kwenda mbio.
9.     Dalili za shinikizo la damu
10.                        Tumbo kuchafuka / kuvimbiwa
11.                        Kupata vipele / kujikuna mwilini
12.                        Kupata mkojo mara kwa mara
13.                        Hali ya mchecheto na kutetemeka
14.                        Kupata mafua mara kwa mara


Mabadiliko kisaikolojia /hisia

1.     Feeling of loss of control
2.     Loss of meaning
3.     Feeling inadequate/incompetent
4.     Forgetful
5.     Resistant to suggestions
6.     Feeling trapped
7.     Difficulty concentrating
8.     Boredom
9.     Feeling work doesn’t fit in with personal values
10.                     Loss of sense of humor
11.                     In denial
12.                     Detached
13.                     Sad
14.                     Fearful/anxious
15.                     Frustrated
16.                     Overwhelmed

Mabadiliko ya mwenendo/ tabia

1.     Kupata ajali mara kwa mara
2.     Kukosa kazini mara nyngi kwa sababu za kiafya
3.     Pumzi ya kina mara kwa mara
4.     Kereka haraka /hasira za karibu
5.     Kutokwa machozi kwa urahisi
6.     Kujitenga
7.     Kutilia mashaka
8.     Mabadiliko katika uhusiano na watu wengine
9.     Kutojali kupuuzia
10.                        Kufanya kazi kwa bidii lakini ufanisi sana
11.                        Kuongezeka matumizi ya dawa, pombe na dawa nyingine kama za usingizi au za kulevya.

Ni nini chanzo cha “Burnout”?

Ø Masuala ya binafsi
Ø Matatizo yatokanayo na mazingira
Ø Masuala ya muundo /mfumo wa kazi

Masuala ya Binafsi

1.     Matatizo ya kiafya
2.     Kukinai /kuchoshwa na majukumu hali halisi
3.     Matatizo ya kifedha
4.     Mazoea ambayo hayana tija
5.     Kuhudumia bila “nafasi ya kupumua”
6.     Kukosa watu wa kutegemea /wanaokujali
7.     Mila na desturi /imani
8.     Ufinyu wa mikakati ya kisakolojia ya kukabiliana na changamoto za maisha
9.     Mahusiano ya usumbufu na kero

Matatizo ya mazingira

1.     Kelele, mwanga mkubwa, joto au baridi kupita kiasi, hewa nzito
2.     Msongo wa kukabiliana na mabadiliko ya teknolojia /kukabiliana na taarifa nyingi mno kwa wakati mmoja
3.     Upungufu au kukosa vitendea kazi
4.     Mazingira hatarishi kazini
5.     Namna unavyokaa kwenye kiti /meza sehemu yako ya kazi
6.     Kuishi maisha ya kusongamana

Masuala ya mfumo au taratibu za kazi

1.     Kazi nyingi mno au kazi kidogo
2.     Majuku yasiyo wazi
3.     Majukumu mengi mno
4.     Kufanya kazi usiyo na ujuzi nayo
5.     Uwajibikaji
6.     Uwezo mkubwa mno kulingana na kazi, au uwezo mdogo
7.     Kutokujua usalama kazini utakuwaje baadaye
8.     Namna utawala unavyoendeshwa
9.     Utamaduni wa sehemu ya kazi
10.                     Mabadiliko ya mara kwa mara
11.                     Uwezekano mdogo wa kupata maendeleo, nafasi ya kuwa mbunifu au kuchangia

Namna ya kuikabili hali ya “Burnout”

1.     Chunguza na uondokane na zile sababu ambazo unafikiri zimekuletea hali ya “Burnout”
2.     Tambua yale ambayo yanawezekana kubadilisha na yale ambayo hayawezekani.
3.     Badili yale yanayowezekana
4.     Jiwekee malengo yanayoendana na yale unayothamini na kuamini kwa dhati.
5.     Weka mipaka iwe wazi kwako ni yapi yanawezekana au kukubalika na yapi hayawezekani.
6.     Wape wasaidizi wako baadhi ya majukumu
7.     Pumzika mara kwa mara, mazoezi, sala, mapumziko ya kutafakari
8.     Jiwekee changamoto mpya ambazo zinaendana na dhamira yako na ambazo zitakufurahisha.
Pata msaada kwingine

Namna ya kujikinga usifikie hali ya “Burnout”

1.     Jizoeshe kutawala akili yako, chunga fikra zako
2.     Pata mlo kamili unaokuongezea ufanisi
3.     Fanya mazoezi ya mwili angalau mara 3 kwa wiki
4.     Ukiona unachoka, jipumzishe
5.     Jifunze kuhimili changamoto za maisha, (kukubali, kufurahia unachofanya na uwe na shauku ya kukifanya vizuri)
6.     Jijengee tabia ya ucheshi na kufurahia ucheshi
7.     Jiwekee mazingira yanayoleta raha na kuchangamsha
8.     Epuka matumizi ya pombe au dawa za kulevya kama tiba ya “burnout”


Tunza akili yako kwa manufaa yako, familia yako, na jamii yako kwa ujumla wake!


Monday, February 24, 2014

VIDEO ya Miriam Njeru: Mama asiye na Mikono na Jinsi anavyojimudu

Ulemavu si kukosa uwezo (Disability is not inability)

Huyu ni mama wa Kikenya, hana mikono yote; kazi zote anatumia miguu badala ya mikono.

Kazi anazoziweza:

1. Kupika
2. Kufua nguo
3. Kumbadilisha nguo mtoto wake
4. Ana taaluma ya stationery
Matatizo anayokabiliana nayo:

1. Mtazamo hasi kwa jamii ya Kikenya kuhusu ulemavu wake
2. Amekosa ajira kwa sababu ya ulemavu wake
3. Marafiki zake walimshauri atoe mimba kisa yeye ni mlemavu

Tufikiri Kijumuishi...... Tutende Kijumuishi........ Tujenge Taifa Jumuishi..